Social Icons

HII

WASILIANA NASI KUPITIA. E-mail: ngambabakari@gmail.com., Namba ya simu +255 657 185 504 Pia waweza kutujuza kwa lolote linalo endelea sehemu uliyopo

kachumbari

kachumbari

Wednesday, October 30, 2013

Mwidau ataka kasi ya maendeleo Tanga

Mbunge Amina Mwidau, akihutubia wanannchi wa Wilaya ya Pangani katika ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo Mkoa wa Tanga. 100_4085Mbunge Mwidau akiwa na Ofisa Utamaduni na Michezo wa Wilaya ya Pangani, Kemmy Anatory mara baada ya kuzindua mashindano ya Mwidau
 CUP.
  100_4112Mbunge Amina Mwidau, akikabidhi vifaa vya michezo kwa kiongozi wa Timu ya soka ya wanawake ya Spin Sister, Habiba Hamisi. Timu hiyo ipo Marizala Pongwe jijini Tanga. 100_4114Mbunge Amina Mwidau, akikabidhi vifaa vya michezo kwa kiongozi wa Timu ya soka ya wanawake ya Spin Sister, Habiba Hamisi. Timu hiyo ipo Marizala Pongwe jijini Tanga.

……………………………………………………………………………………
Na Mwandishi Wetu, Tanga
MBUNGE wa Viti maalum Mkoa wa Tanga Amina Mwidau (CUF), amewataka wananchi wa Mkoa wa Tanga kubadilika kwa kuwa na ari ya kujiletea maendeleo yao na jamii kwa ujumla.
Kauli hiyo ameitoa mjini hapa alipokuwa akizungumza na vionozi wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Tanga (Tanga Press Club).
Alisema kuwa ili maendeleo ya haraka yaweze kupatikana katika mkoa huo ni lazima jamii kubadili kwa kuwa na mawazo chanya.
“Maendeleo ni jambo muhimu sana na katika hili ni lazima tushirikiane kwa dhati. Binafsi ninapenda kupongeza juhudi za chama cha Waandishi wa habari Mkoa wa Tanga kwa kazi kubwa na nzuri wanayofanya katika kutangaza mkoa wetu.
“Nilikuwa nasoma na sasa kila wakati tutakuwa pamoja na wanahabari pamoja na wananchi wa mkoa wetu ili kuweza kuungana kwa pamoja katika juhudi za maendeleo za mkoa,” alisema Mwidau
chanzo fullshangwe.

No comments:

Post a Comment