Social Icons

HII

WASILIANA NASI KUPITIA. E-mail: ngambabakari@gmail.com., Namba ya simu +255 657 185 504 Pia waweza kutujuza kwa lolote linalo endelea sehemu uliyopo

kachumbari

kachumbari

Tuesday, November 5, 2013

Mama amuua mtoto mchanga kwa sumu ya panya

Msichana wa miaka 14 jina limehifadhiwa,anashikiliwa na jeshi la polisi mkoani Pwani kwa tuhuma ya kumuua mtoto wake Mariam Stamili mwenye miezi tisa kwa kisingizio cha ugumu wa maisha.

Kamanda wa Polisi Pwani Ulich Matei amedhibitisha tukio ambapo amesema limetokea huko Mlandizi Kibaha na kwamba mama huyo anadaiwa kumuua mtoto wake huyo baada ya kumnywesha sumu inayodhaniwa ni ya kuulia panya.

Amesema mama huyo alifikia uamuzi wa kumnywesha sumu ya panya mtoto huyo akiwa nyumbani kwake Mlandizi na muda mfupi alipoona hali ya kichanga hicho inakua mbaya alimpigia simu mzazi mwenzake baba wa mtoto Stamili Shaban (21)na kumueleza kuwa anaumwa sana.

Baba mtoto alifika kumjulia hali mwanaye na kweli alimkuta ana hali mbaya na mke wake kumueleza kuwa kichanga hicho kinasumbuliwa  dege dege hivyo walikubaliana kwenda kumtafutia matibabu. 

Hata hivyo wazazi hao walimpeleka kwa mganga wa kienyeji huko Kijiji cha Disunyara ambapo marehemu alianza kupatiwa matibabu lakini hali yake ilizidi kuwa mbaya na kulazimika kumuhamishia kituo cha afya Mlandizi ambapo 
alifariki dunia kabla hata ya kuanza tiba.

Matei ameongeza kuwa uchunguzi wa awali katika kituo cha afya hicho umebaini kuwa chanzo cha kifo hicho ni kunyweshwa  sumu inayosadikiwa kuwa ni ya panya .

Amebainisha kuwa uchunguzi zaidi umebaini siku ya tukio mtoto huyo hakuwa na ugonjwa wowote bali mama yake aliamua kununua sumu hiyo na kumnyweshwa na hali ilipobadilika alimpigia simu mume wake na kumueleza  mtoto wao anasumbuliwa na degedege .

Mwili wa marehemu umechukuliwa na ndugu 
na kuzikwa  huko Kijiji cha Kilangalanga, 
huku majirani wakishuhudia mama huyo akilia na kusema chanzo cha kifo ni yeye mwenyewe na si degedege kama alivyosema awali,hivyo asamehewe.

Matei amesema mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma dhidi yake baada ya upelelezi kukamilika.

No comments:

Post a Comment