Social Icons

HII

WASILIANA NASI KUPITIA. E-mail: ngambabakari@gmail.com., Namba ya simu +255 657 185 504 Pia waweza kutujuza kwa lolote linalo endelea sehemu uliyopo

kachumbari

kachumbari

Wednesday, November 20, 2013

Picha za uzinduzi wa safari za ndege ya Auric Air kati ya Dar es Salaam na Morogoro


Auric Air kwenye uwanja wa ndege Morogoro
Shirika la ndege la Auric Air mwishoni mwa wiki limefanikiwa kuzindua safari safari za kila siku za ndege kati ya Morogoro na Dar es salaam ikiwa ni katika utekelezaji wa ahadi yake katika kuchangia maendeleo ya sekta ya usafiri wa anga nchini.


Katika uzinduzi huo ambao mgeni rasmi alikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Joel Bendera ambaye anaelezea kuzinduliwa kwa safari hizo kutasaidia kuukuza mji wa Morogoro kiuchumi, kupitia sekta ya utalii, na hatimaye kuongeza kasi ya mikakati iliyopo ya kuufanya mji huo kuwa jiji.

“Ni fursa sasa kwa wananchi wa morogoro kukuza biashara zao
Kutokana na kurahisishwa mawasiliano kati ya mikoa hiyo miwili, na hata
Wagonjwa kufuata kwa haraka huduma za rufaa na kitabibu” anasema Bendera.

Auric Air katika taarifa yake kwenye mtandao wa facebook imeeleza wazi lengo la kuzindua kwa safari hizo kuwa pamoja na kuukuza uchumi pia itachochea maendeleo ya mkoa kwa ujumla.


“Tuta safiri kila siku,kuondoka morogoro saa 12:30 (alfajiri) asubuhi na kutoka dar es salaam saa 11:15 jioni kwa kutumia ndege yetu yenye uwezo wa kubeba habiria 13 kwa safari moja ambapo safari hiyo itachukua dakika 35” inaeleza taarifa hiyo

Shirika hilo linasema limejipanga mathubuti katika safari hizo na kuahidi kutoa huduma hiyo kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zote ili kuendeleza sifa yake ya kuwa shirika lenye huduma bora za usafiri wa anga nchini.

Auric Air pia inatarajia kuongeza safari zake kutoka Dar es salaam, kupitia Ifakara hadi Songea kwa kwa lengo la kuwafikishia huduma hiyo watanzania katika mikoa yote.

Tazama picha zaidi za uzinduzi ulivyokuwa

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Joel Bendera akishuka kwenye ndege ya Auric Air wakati wa uzinduzi wa safari za ndege kati ya Dar es Salaam na Morogoro

Meya wa Manispaa ya Morogoro, Amir Nondo akipanda kwenye ndege ya Auric Air

Tabianch blog

No comments:

Post a Comment