Social Icons

HII

WASILIANA NASI KUPITIA. E-mail: ngambabakari@gmail.com., Namba ya simu +255 657 185 504 Pia waweza kutujuza kwa lolote linalo endelea sehemu uliyopo

kachumbari

kachumbari

Monday, December 2, 2013

AJALI MBAYA YA MALORI YATOKEA LEO MTO WAMI MKOA WA PWANI LEO



Ajali mbaya iliyohusisha magari mawili makubwa (malori) imetokea leo katika eneo na mteremko wa mto Wami,Mkoani Pwani na kupelekea msongamano mkubwa wa magari mengine yakiwemo mabasi yaendayo mikoa ya Tanga,Kilimanjaro na Arusha pamoja na yale ya nchi jirani.

Chanzo cha ajali hiyo inadaiwa kuwa ni kufeli kwa breki kwa moja ya malori hayo yakiwa yanateremka kwenye mlima huo.Askari Polisi wapo eneo la tukio kuhakikisha usalama unapatikana na kutafuta namna ya kuyapitisha magari mengine.haijafahamika ni watu wangapi wamepoteza maisha ama kujeruhiwa.

Pichani ni Malori hayo yaliyogongana yakiwa yameziba njia baada ya kugongana eneo la mto wami.Picha na Mdau wa Globu ya Jamii alie safarini.

No comments:

Post a Comment