Social Icons

HII

WASILIANA NASI KUPITIA. E-mail: ngambabakari@gmail.com., Namba ya simu +255 657 185 504 Pia waweza kutujuza kwa lolote linalo endelea sehemu uliyopo

kachumbari

kachumbari

Friday, March 28, 2014

SERIKALI KUTAZAMA ENEO ITAKAPO JENGWA BANDARI YA MWAMBANI

Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga, Freddy Liundi (wa pili kutoka kushoto) akitoa maelezo juu ya maendeleo ya mradi wa ujenzi wa Bandari ya Mwambani kwa kiongozi wa timu ya wakaguzi wa miradi ya maendeleo  kutoka Tume ya Mipango ambaye ni Naibu Katibu Mtendaji anayesimamia Kongane ya Sekta za Uzalishaji, Bw. Maduka Kessy.Timu ya wakaguzi wa miradi ya maendeleo, kutoka Tume ya Mipango wakiongozwa na Naibu Katibu Mtendaji, Bw. Maduka Kessy (wa kwanza kushoto) wakipata maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa bandari ya mwambani ambapo upembuzi yakinifu tayari umeshafanyika.


Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga akionesha eneo ambapo bandari ya Mwambani itajengwa.

Picha ikionesha eneo la mwambani ambako ndipo miundombinu ya bandari itajengwa

Timu ya wakaguzi wa miradi ya maendeleo kutoka Tume ya Mipango wakisikiliza maelezo kutoka kwa Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga, Bw. Freddy Liundi (wa pili kulia) ufukweni mwa bahari, eneo ambapo bandari ya Mwambani itajengwa.


Picha na Joyce Mkinga

No comments:

Post a Comment