Muigizaji mkongwe nchini, Said Ngamba maarufu kwa jina la
Mzee Small amefariki dunia usiku huu akiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili
jijini Dar. Mzee Small amefariki kwa ugonjwa wa presha baada ya kuugua kwa muda
mrefu kabla ya kuzidiwa jana na kupelekwa Muhimbili. Mtoto wa marehemu aitwaye,
Muhidin amethibitisha kifo cha Mzee Small.
YANAYOENDELEA KUJIRI NYUMBANI KWA MAREHEMU MZEE SMALL
Waombolezaji wakiwa na simanzi nyumbani kwa marehemu Said
Ngamba 'Mzee Small' aliyefariki usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Taifa
jijini Dar es Salaam.
(PICHA NA SHANI RAMADHAN, GLADNESS MALLYA NA GABRIEL NG'OSHA)
No comments:
Post a Comment