Social Icons

HII

WASILIANA NASI KUPITIA. E-mail: ngambabakari@gmail.com., Namba ya simu +255 657 185 504 Pia waweza kutujuza kwa lolote linalo endelea sehemu uliyopo

kachumbari

kachumbari

Tuesday, September 2, 2014

AGONGWA NA DALADALA ENEO LA UBUNGO MAJI JIJINI DAR

 Wasamalia wema wakijaribu kuokoa maisha ya dada aliyegongwa na gari (daladala) maeneo ya Ubungo maji wakati akivuka barabara. 
Mwanamke mmoja (jina halijafahamika) aliyekuwa anavuka barabara ya Morogoro maeneo ya Ubungo maji kutoka ng'ambo ya tank na kuelekea upande wa Tanesco amegongwa na gari ya daladala aina ya Toyota Coaster lililodaiwa kuvunja sheria likiwa  linapita kwenye barabara ya magari ya mwendo kasi. Katika ajali hiyo dereva wa basi(daladala) hakupatikana kwani alikimbia baada ya ajali.
 Majeruhi (dada huyo) akichukuliwa kwenye gari na wasamaria wema.
HiIi ndilo gari aina ya Toyota Coaster lenye namba za usajili T454 BBV lililomgonga dada huyo.
Mmoja wa mashuda wa ajali ameiambia blog hii ya Pamoja kuwa mama huyo alipogongwa na daladala lá inayofanya kazi zake kutoka Mbezi - Muhimbili alafu likamburuza yapata mita kumi na tano, baada ya daladala kusimama yule mama akawa anajitahidi kutoka pale uvunguni  lakini ilishindikana na damu zilikuwa zinavuja kichwani. Mpaka walipo shuka abiiria wote waliokuwa wamepanda daladala hiyo na kuliinua na kumtoa mama huyo kwenye daladala ,na baada ya kutokea ajali hiyo dereva wa daladala hiyo alikimbia.

No comments:

Post a Comment