Baadhi ya wananchi wa mjini Iringa na abiria wa basi la Embakasy wakitazama basi hilo lililopinduka leo eneo la Ipogolo mjini Iringa .
Abiria wakiwa wanatzama ajali hiyo mara baada ya kunusurika katika basi walilokuwa wakisafiria
wasamalia wema wakiwa wanasaidia kutoa mizigo iliyokuwepo katika basi
AJALI yanua mmoja Iringa huku abiria 18 wakinusurika kifo baada ya basi la kampuni
ya Embakasy lenye namba za usajili T 997 AKJ kuacha njia ya
kupinduka eneo la Ipogolo mjini Iringa.
Wakizungumza
na mtandao huu eneo la ajali baadhi ya
abiria wa basi hilo walidai kuwa basi hilo lilikuwa likitaka
kuingia katika kituo kimoja wapo cha mafuta eneo hilo na wakati
likitoka ndipo liliponusurika kugongana na lori lililokuwa barabara
kuu ya Iringa - Mbeya .
Hivyo kutokana na kunusuri
kugongana ndipo dereva wa basi hilo alipoamua kulikwepa lori hilo
kwa kukata kuna kubwa zaidi iliyopelekea basi hilo kuacha njia
na kupinduka kando ya barabara hiyo .
konda
wa basi hilo Bw Esack Mtandi alielezea tukio hilo alisema
kuwa basi hilo lilikuwa likitaka kuingia kujaza mafuta katika
kituo kimoja wapo cha mafuta kilichopo eneo hilo na mbele kulikuwa
na lori na wakati dereva akijiandaa kuingia kituoni hapo
ghafla usukani uligoma na hivyo kumtoa dereva nje ya barabara kabla
ya kupinduka .
Alisema katika basi hilo kati ya
abiria 18 waliokuwepo abiria 6 ndio waliojeruhiwa akiwemo dereva
na hakuna aliyepoteza masisha .
Kwa upande wake jeshi
la polisi mkoani Iringa limethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na
kuwa ajali hiyo ilitokea majira ya saa 3 kasoro asubuhi ya leo na
kumtaja dereva wa basi hilo kuwa ni Abdalah Nyalusi
Alisema kamanda wa polisi mkoa wa Iringa Ramadhan Mungi na kuwa katika ajali hiyo hakuna abiria aliyepoteza maisha .
Wakati
huo huo mmoja kati ya wafanyabiashara maarufu mji wa Ilula
wilayani Kilolo mkoani hapa aliyefahakika kwa jina moja la kasim
aliyekuwa akiendesha gari lenye namba za usajili T 111 GRE RAV4
amekufa papo hapo baada ya kugongana uso kwa uso la lori .
Kamanda
Mungi alisema kuwa mfanyabiashara huyo alikuwa akitokea Ilula
kuja Iringa mjini na baada ta kufika eneo la kona ya Igumbilo
barabara kuu ya Iringa - Dar es salaam wakati akijaribu kulipita
daladala lililokuwa mbele yake katika kona hiyo ghafla alikutana
na lori hilo na kugongana nalo .
Hata hivyo
alisema jina kamili la mtu huyo bado kufahamika na kuwa
wanasubiri ndugu zake ili kujakutambua mwili huo na kutoa jina
kamili.
hiyo habari umeandika au umeandikiwa ndugu?
ReplyDelete