Social Icons

HII

WASILIANA NASI KUPITIA. E-mail: ngambabakari@gmail.com., Namba ya simu +255 657 185 504 Pia waweza kutujuza kwa lolote linalo endelea sehemu uliyopo

kachumbari

kachumbari

Wednesday, December 18, 2013

BREAKING NEWZZZ ;;;Tazama picha za tukio laPANTON YA MV MAGOGONI YAKOSA MUELEKE KIGAMBONI YAELEKEA KURASINI ABIRIA WAKAA KWA MUDA WA SAA MOJA NA NUSU,ZAIDI


PANTON YA MV MAGOGONI YAKOSA MUELEKE KIGAMBONI YAELEKEA KURASINI ABIRIA WAKAA KWA MUDA WA SAA MOJA NA NUSU,ZAIDI SIKILIZA JAHAZI LA CLOUDS FMHabari kamili 

Ilikuwa ni mida ya saa nane mchana ambapo Pantoni kubwa ya Mv. Magogoni ikiwa imesheheni abiria ikiwavusha kutokea Posta kuelekea Kigamboni , ilipatwa na wakati mgumu baada ya kushindwa kutia nanga ili iweze kusimama na abiria waweze kushuka..
Tukio hilo ambalo chanzo chake kimetokana na Injini za Pantoni hilo kushindwa kufanya kazi  haikuweza kutia nanga kwa muda wote huo.. na ambapo kulikuwa na upepo mkali sana ambao ulisababisha  Pantoni hiyo kukosa muelekeo na kuanza kuambaa ambaa mpaka maeneo ya Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere kisha kusukumwa zaidi hadi eneo la bandari ya Zanzibar.
Hata hivyo baada ya hali kuzidikuwa si nzuri walilazimika kuita meli ndogo za uokoaji ambapo meli ya kwanza haikuweza kuvuta pantoni hiyo na kulazimika kuongeza meli nyingine ili iweze kuongeza nguvu pamoja na boti za Jeshi la polisi ambazo zote zilifika na kwa ushirikiano mkubwa ziliweza kufanikiwa zoezi hilo la kuirudisha pantoni hiyo katika eneo lake husika. 
Na abiria ambao walinusurika kuweza kushuka na kuendelea na shughuli zao za kawaida..
 Baadhi ya Abiria katika Pantoni ya Mv. Magogoni wakiwa katika mshangao jinsi kivuko hicho kinavyo pepea pepea
 Abiria wakiwa wamevaa mavazi maalumu ya kujiokoa na kujiweka sawa kama kungetokea hatari yoyote 
wasafiri wakiwa wamejiandaa kwa kuvaa  life jacket kwaajiri ya usalama zaidi
Wasafiri wakiwa na hofu ndani ya pantoni
baadhi ya abiria wakionekana kuwa na hofu
kutokana na pantoni hilo kupoteza muelekeo
 Ilikuwa ni baada ya kuanza kuvutwa na Meli zengine kuelekea katika eneo la kushukia, ambapo kila mtu alikua anaonekana mwenye nyuso ya furaha kuashiria kuokoka katika hatari.


Pantoni ya Mv. Magogoni ikiwa imetulia sasa na abiria wakiwa wanajiandaa kushuka.
Picha zote na Dar es salaam yetu Blog

No comments:

Post a Comment