Social Icons

HII

WASILIANA NASI KUPITIA. E-mail: ngambabakari@gmail.com., Namba ya simu +255 657 185 504 Pia waweza kutujuza kwa lolote linalo endelea sehemu uliyopo

kachumbari

kachumbari

Monday, April 14, 2014

GURUMO AFARIKI DUNIA MAZISHI KESHO

Gurumo.              
Mwanamuziki mkongwe pengine kuliko wote kwa sasa nchini na mwasisi wa Bendi ya Msondo Ngoma, Muhidin Maalim Gurumo amefariki dunia jana katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), alipokuwa akipatiwa matibabu ya moyo.
Akizungumza jana mtoto wa kwanza wa marehemu Abdallah Muhidin alisema baba yake alizidiwa juzi na kupelekwa Muhimbili ambako aliendelea na matibabu hadi mauti yalipomkuta jana mchana.
“Alianza kuugua wiki tatu zilizopita, mwishoni hali ilianza kubadilika akawa kila akila chakula anatapika. Hali yake ilianza kubadilika, alipelekwa Muhimbili kwa matibabu,” alisema.
Alisema muda mrefu marehemu alikuwa akisumbuliwa na tatizo la mapafu, shinikizo la damu na moyo. Marehemu ameacha mjane na watoto sita.
Abdallah alisema marehemu atazikwa leo Masaki, Kisarawe na ataagwa leo adhuhuri nyumbani kwake Mabibo External, Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Chama cha Muziki wa Dansi Tanzania (Chamudata), Kassim Mapili alisema chama chake kimempoteza kiongozi wake kwani hadi kifo chake, Gurumo alikuwa Mkuu wa Idara ya Fedha.
Desemba 14 mwaka jana wanamuziki wa dansi wakishirikiana na wanamuziki wa kizazi kipya, walishiriki pamoja katika tamasha la kumuaga nguli huyo baada ya kutangaza rasmi kustaafu muziki akiwa amedumu kwa miaka 53. Hadi kustaafu kwake, Gurumo alizitumikia pia bendi za Kilimanjaro Chacha, Rufiji Jazz, Kilwa Jazz, Sikinde na OSS. 

Pia alikuwa kiongozi na mmoja wa wamiliki wa Msondo Ngoma ambayo hapo awali ilijulikana kwa majina ya Nuta, Juwata na Ottu. Gurumo ameitumikia Bendi ya Msondo katika majina yote ya nyuma

No comments:

Post a Comment