Social Icons

HII

WASILIANA NASI KUPITIA. E-mail: ngambabakari@gmail.com., Namba ya simu +255 657 185 504 Pia waweza kutujuza kwa lolote linalo endelea sehemu uliyopo

kachumbari

kachumbari

Wednesday, May 28, 2014

MWILI WA MAREHEMU RECHO WA BONGO MOVIE KUAGWA KATIKA VIWANJA VYA LEADERS NA KUZIKWA KESHO HAPA DAR

Steve Nyerere akijadili jambo na wasanii wenzake

Msanii wa filamu Rachel Haule aliyefariki usiku wa kuamkia jana katika hospitali ya Muhimbili jijini Dar es Salaam anatarajiwa kuagwa siku kesho Alhamis katika viwanja vya Leaders Club na kuzikwa siku hiyohiyo katika makaburi Kinondoni.
Akizungumza na mtandao huu jana mwenyekiti wa bongomovie Steve Nyerere amesema kuwa bado wapo kwenye mikakati ya kukusanya michango itakayosaidia shughuli hiyo.
“Tulikuwa tunachangishana pesa ili kuwezesha suala la msiba,tunashukuru Mungu mambo yameenda salama, suala la kuaga ,tutaaga siku ya alhamisi pale Leaders na baada ya hapo tutaelekea katika makaburi ya Kinondoni kwenda kumzika ndugu yetu, “alisema.

No comments:

Post a Comment