




Kwa mujibu wa mganga huyo ambaye anasaidiwa na Athman Keneth(30) mkazi wa Chunya mkoani hapa, alisema Chatu huyo ni mdogo na juhudi za kuendelea kumtafuta mkubwa zitaendelea kama kweli yupo.
Alisema mara nyingi Chatu mdogo anapoonekana Mkubwa anakuwa amehama ili kuwapisha wadogo kuendelea na maisha yao ama huyo mdogo alisombwa na maji kipindi cha mvua kutoka kwenye hifadhi na wenzie.
Hata hivyo taarifa kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji zinadai kuwa baada ya kukamatwa kwa Chatu huyo atahifadhiwa na kutunzwa katika Hifadhi ya Wanyama ya Ifisi ambako kuna wanyamapori wengine wa maonesho.
No comments:
Post a Comment