Social Icons

HII

WASILIANA NASI KUPITIA. E-mail: ngambabakari@gmail.com., Namba ya simu +255 657 185 504 Pia waweza kutujuza kwa lolote linalo endelea sehemu uliyopo

kachumbari

kachumbari

Saturday, May 17, 2014

NEWSS:MSANII MAARUFU WA FILAM ADAM KUAMBIANA AFARIKI DUNIA LEO TAARIFA ZOTE SOMA HAPA

Taarifa za awali kuhusu kifo cha Director Maarufu wa Bongo Movie Adam Kuambiana
DSC02051
Hizi ni taarifa zingine za ghafla ambazo Tanzania tumezipokea kwa mshtuko na masikitiko ni kifo cha miongoni mwa-madirector wa Tanzania ambao ni waigizaji pia,huyu ni Adam Kuambiana ambaye taarifa za kifo chake zimeanza kusambaa mchana wa Mei 17.
Mwili wa Marehemu Adam Kuambiana ukitolewa nje ya Hospitali  ya Mama Ngoma iliyopo Mwenge jijini Dar es Salaam kupelekwa katika Hospitali ya Muhimbili kutunzwa 
Mwili wa Marehemu Adam Kuambiana ukiwekwa kwenye gari tayari kupelekwa Muhimbili kuhifadhiwa.
DSC00263
Marehemu Adam Kuambiana akiwa location enzi za uhai wake.
Mwenyekiti wa Bongo Movie Steve Nyerere amesema>>’Mwenzetu Adam Philipo Kuambiana amefariki akiwa Location ana shoot,mimi nimepigiwa simu saa 3 asubuhi kuwa hospitali pale Mwenge niende nikahakikishe kuwa ni kweli Adam amefariki na kweli kufika pale nikamkuta Adam Kuambiana amefariki’
‘ tumetoka Muhumbili kwenda kumsitiri mwenzetu,taarifa inasema wakati yupo location alikua analalamika tumbo linamuuma linamuuma kumfikisha hospitali ndipo umauti ukamfika’.
Kwa mujibu wa Steve Nyerere amesema kuwa marehemu Adam kuambiana alikua ana shoot filamu yake mpya ambayo ndani yake 

amewashirikisha wasanii kadhaa wa Bongo fleva akiwemo Q Chillah,taratibu za mazishi na msiba kwa ujumla

No comments:

Post a Comment