Social Icons

HII

WASILIANA NASI KUPITIA. E-mail: ngambabakari@gmail.com., Namba ya simu +255 657 185 504 Pia waweza kutujuza kwa lolote linalo endelea sehemu uliyopo

kachumbari

kachumbari

Monday, July 28, 2014

GARI YA PATA AJALI NA KUINGIA MTARONI JIJINI MBEYA LEO

Wasamalia wema wakijaribu kulinasua gari aina ya Toyota Corolla (namba zake za  usajili hazikuweza fahamamika mara moja kutokana na kutokuwepo)  lililoingia kwenye mtaro baada ya dereva wake kuzidiwa maarifa ya  kiudereva na kujikuta akiingia mtaroni,katika eneo la Mafiat mkabala na  kituo cha mafuta cha Oilcom jijini Mbeya asubuhi hii.

Dereva wa Gari hilo pamoja na mtu mwingine mmoja wamejeruhiwa na kukimbizwa hospital kwa  matibabu.Chanzo cha ajali hiyo inaelezwa ni mwendo kasi aliokuwa nao  Dereva wa gari hilo.
Wasamalia wema hao wakiangalia namna ya kuweza kulichomoa gari hilo.
Hayaaaa..... Moja.... mbili.... tatuuu twendeeeeeeee......
Mara wakafanikiwa kulitoma kwenye mtaro huo.Picha na Fadhil Atick,Mbeya

No comments:

Post a Comment