Social Icons

HII

WASILIANA NASI KUPITIA. E-mail: ngambabakari@gmail.com., Namba ya simu +255 657 185 504 Pia waweza kutujuza kwa lolote linalo endelea sehemu uliyopo

kachumbari

kachumbari

Tuesday, July 1, 2014

PICHA ZA KITUO KIPYA CHA MABASI NANE NANE KILICHO ZINDULIWA LEO KIKIWA NA MAPUNGUFU MENGI.

 Mabasi yakiwa yamepaki katika kituo kipya cha mabasi Nanenane
 Hili eneo ambalo kuna Manyasi ni eneo ambalo limetengwa maalum kwa ajili ya kuweka sehemu ya abiria kungojea usafiri au walio na wageni kungojea watu wao lakini hakuna kilicho jengwa , hali inayosababisha usumbufu mkubwa.
 Baadhi ya Abiria na watu wanaongoja ndugu zao wakiwa wamekaa katika  manyasi huku wakiwa hawana eneo maalum la wao kukaa, jambo ambalo linasababisha wapigwe na jua pia Mvua ikinyesha hakuna pa kujihifadhi.
 Madereva na makonda wakiwa katika eneo hilo jipya la kituo cha basi
 Abiria wakiwa wamekaa tuu bila mpangilio
Biashara zinaendelea 


Swali linakuja hapa kwa Halmashauri ya Jiji, Je wakati kituo hiki cha basi kinazinduliwa hamkuona kuwa kunatakiwa kuwe na sehemu ya mapumziko? Wananchi wanaomba muwawekee eneo la mapumziko kulipo kuendelea kukaa katika majani ambayo hata hivyo yatakuwa mavumbi siku chache zijazo

No comments:

Post a Comment