Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto Mhe
Ummy Mwalimu
Idadi ya watu waliofariki kutokana na kuugua ugonjwa
wa ajabu ulioripotiwa mkoani Dodoma, imefikia 11.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto, Ummy Mwalimu, alisema hayo jana katika taarifa yake aliyoituma kwa
vyombo vya habari kupitia kurugenzi ya mawasiliano ya wizara hiyo.
Alisema kwamba, idadi ya walioripotiwa kuugua ugonjwa
huo nayo imeongezeka na kufikia 43 hadi kufikia Julai 3, mwaka huu baada ya
ugonjwa huo kuripotiwa Juni 13 mwaka huu.
“Ugonjwa huo uliripotiwa Juni 13, mwaka huu wilayani
Chemba, Mkoa wa Dodoma na hadi kufikia jana (juzi), kulikuwa na wagonjwa 43 na
vifo 11, Mbali na Mkoa huo wa Dodoma, Mkoa wa Manyara nao umeripotiwa kuwa
na wagonjwa wa aina hiyo"
“Katika Halmashauri ya Chemba, kumeripotiwa kuwepo
wagonjwa 34, Kondoa wanne, Dodoma Manispaa mmoja, Chamwino mmoja na Kiteto
watatu. Vifo 10 viliripotiwa katika Halmashauri ya Chemba na kifo kimoja
kiliripotiwa katika Halmashauri ya Kiteto,” alisema Ummy katika taarifa
hiyo"
Pamoja na hayo, alisema uchunguzi wa awali wa
kimaabara uliofanywa kwa baadhi ya vyakula walivyotumia wagonjwa, ulibaini kuwa
vyakula hivyo vilikuwa na sumu kuvu iitwayo aflatoxins.
No comments:
Post a Comment