Mgeni rasmi ambaye ni Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira akikagua Gwaride la Wahitimu wa Mafunzo ya Awali ya Uaskari Magereza, Kozi Na. 28 ya Mwaka 2016.
Wahitimu wa
Mafunzo ya Awali ya Uaskari Magereza, Kozi Na. 28 ya Mwaka 2016 wakila
kiapo cha Utii kwa Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama
ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama inavyoonekana katika
picha wakiwa wakakamavu.
Mgeni rasmi akimkabidhi cheti cha sifa mmoja wa Askari Wahitimu ambaye
amefanya vizuri zaidi katika nyanja ya Nidhamu katika kipindi chote cha Mafunzo
hayo.
Gadi Maalum ya Gwaride la
kunyakua iliyoundwa na Wahitimu wa Mafunzo ya Awali ya Uaskari Magereza wakitoa
heshima mbele ya Jukwaa la Mgeni rasmi ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo
ya Ndani ya Nchi(hayupo pichani).
Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza
wakifuatilia kwa karibu Maonesho mbalimbali katika Uwanja wa Gwaride kwenye
hafla ya kufunga Mafunzo hayo.
Wakufunzi kutoka Kikosi Maalum cha Kutuliza
Ghasia Magerezani(KMKGM) wakionesha onesho la kijasiri kama inavyoonekana
katika picha.
Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP - John Casmir Minja akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi kutoa hotuba yake ya kufunga rasmi kwa Mafunzo ya Awali ya Uaskari Magereza katika Chuo cha Magereza, Kiwira Mbeya.
Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP - John Casmir Minja(wa pili kulia)akiwa ameongozana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi(wa pili kushoto) mara baada ya sherehe za kufunga Mafunzo ya Awali ya Uaskari Magereza, Chuo cha Magereza, Kiwira Mbeya(wa kwanza kulia) ni Mkuu wa Chuo cha Magereza - Kiwira, SACP. Stanford Ntirundura(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira(katikati) katika Jukwaa akipokea
Salaam kutoka kwa Gwaride la Wahitimu wa Mafunzo ya Awali ya Uaskari
Magereza(hawapo pichani) katika hafla ya kufunga Mafunzo hayo leo Julai 9, 2016
Chuo cha Magereza, Kiwira Mbeya. Kushoto ni Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP-
John Casmir Minja.
No comments:
Post a Comment