Social Icons

HII

WASILIANA NASI KUPITIA. E-mail: ngambabakari@gmail.com., Namba ya simu +255 657 185 504 Pia waweza kutujuza kwa lolote linalo endelea sehemu uliyopo

kachumbari

kachumbari

Wednesday, February 12, 2014

NYUMBA YATEKETEA KWA MOTO KILWA MASOKO USIKU WA KUAMKIA LEO





muonekano wa nyumba baada ya moto huo kuzima

Na Abdulaziz Ahmeid,Kilwa Masoko 

Familia moja ya Bw Bernad Towele dereva wa Gari la Takukuru Wilayani Kilwa Imenusurika baada ya Nyumba waliyokuwa wakiishi kuteketea kwa moto usiku wa kuamkia katika mji mdogo wa kilwa masoko.

Akithibitisha kutokea kwa tukio la Ajali hiyo iliyotokea majira ya saa 6 usiku kuamkia leo,Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi,Joseph Mfungomara alieleza kuwa chanzo cha Moto huo bado hakijajulikana ila hakuna majeruhi.

Kamanda Mfungomara alimalizia kuwa Vitu vyote vilivyomo katika nyumba hiyo vyenye thamani ya Tshs 7,700,000/ Havikuweza kuokolewa.

Baadhi ya Wananchi waliopo katika mji huo Akiwemo Mfanya biashara Ahmaid Shukra na Saidi Timamy mmiliki wa kituo cha Mafuta cha Alsat wameiomba Halmashauri hiyo kupeleka ombi maalum serikalini ili waletewe gari la Zimamoto kutokana na wilaya hiyo kuanza uwekezaji unaotokana na Raslimali ya Gesi ya Songosongo pamoja kukua kwa mji huo mashuhuri Afrika ya Mashariki
Chanzo;Michuzi blog


No comments:

Post a Comment